Maziwa ya mama yana virutubisho vyote.

Picha:Afisa lishe jiji la Mwanza Emma Kilimali


Na.Lucy Sanka@cfjmedia
Wanawake Katika Jiji La Mwanza Wameaswa  Kuwanyonyesha Watoto Wao Miezi Sita Ya Mwanzo Pale Anaopojifungua Ili Mtoto Apate Kinga Mwilini Dhidi Ya Maradhi Mbalimbali Na Kukua Katika Msingi Bora.
Hayo Yamesemwa Na Afisa Lishe Katika Jiji La Mwanza Bi Emakilimali  Ofisini Kwake Alipokuwa Akizungumza Na Waandishi Wa Habari Ameeleza Kuwa Imebainika Kuwa Wamama Wengi Siku Hizi Hawazingatii Masharti Ya Kunyonyesha Watoto Wao Badala Yale Wamekuwa Wakinyonyesha Kwa Mazoea Bila Kuzingatia Utaalamu Wa Kiafya.
Aidha Bi Ema Kilimali Ameeleza Kuwa Mama Akimnyonyesha Mtoto Wake Kwa Kuzingatia Utaalamu Wa Afya Mtoto  Atakua Kiakili Vizuri Lakini Pia Kuepusha Gharama Ya Kununua Maziwa Mbadala Na Kuepuka Hata Uchafuzi Wa Mazingira Kutokutupa Makopo Ya Maziwa Ovyo.
Mbali Na Hayo Amewataka Wanawake Wanaonyonyesha Na Wanaotarajia Kunyonyesha Siku Za Karibuni Wawanyonyeshe Watoto Wao Vizuri Waache Kujidanganya Kuwa Akinyonyesha Mtoto Ata Haribu Shepu Yake Atakapo Nyonyesha.
Ikumbukwe Kuwa Kila Ifikapo Tarehe Moja Mwezi Wa Nane Hadi Tarehe Saba Mwezi Wa Nane Ni Wiki Ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama ambayo huadhimiswa Kila Mwaka Ulimwenguni Kote.


0 Comments:

Post a Comment