MWANZA:YAADHIMISHA SIKU YA SELI MUNDU



Pich:Wananchi wakipatiwa elimu juu ya ugonjwa wa seli mundu.


Na.Cornelius F. shija @CFJMEDIA TZ.
Mkoa wa mwanza leo19.june umeungana na mataifa mengine duniani katika maadhimisho ya  ugonjwa wa siko seli pamoja na kutoa semina kwa wazazi ili kutambua  maana ya ugonjwa wa seli mundu  namna ya kupata vipimo pamoja na matibabu yake.
akizungumza katika maadhimisho hayo mganga  bingwa wa watoto dr.emmanuela ambrous amesema kuwa ugonjwa wa seli munu umekuwa tishio kubwa kwa watoto na kuwataka wazazi pamoja na jamii kujenga mazoea ya kupima ugonjwa huo

akizungumza  mmoja  wa wazazi bi. juliana  kutokea nyegezi amesema kuwa  hakutambua mara moja juu ya ugonjwa wa mwanae  unaomsumbua kwa kuwa dalili zilifanana na malaria pia amewaomba wababa wasiwalaumu wake zao juu ya ugonjwa huo kuwa wao ndio chanzo.
nae elikana nyanda pamoja na wadau mbalimbali wamezungumzia juu ya ugonjwa huu pia elikana kama kijana  amejikita  kuzungumzia uzoefu wa kuishi na ugonjwa siko seli katika maeneo ya kazi ,jamii na shuleni kwa miaka 32,

aidha pia  dr. emmanuela ametoa rai kwa jamii kuacha dhana  hiyo potofu iliyopo ya kuhani siko sekli kwa mtoto inasababishwa na mama pekee, bali wazazi wote mmoja akiwa na vimelea na mwingine akiwa na siko seli

TAZAMA VIDEO:MAMA MWENYE MTOTO WA SIKO SELI






0 Comments:

Post a Comment